MITI 200 YAPANDWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MAWENI

Posted on: February 8th, 2023

Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango miji, Ujenzi na Mazingira na Diwani wa Kata ya Kitongoni iliyopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Himidi Omary Himidi amepongeza uongozi wa  Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa Maweni - Kigoma kwa kusimamia na utunzaji wa Mazingira.

Pongezi hizò amezitoa Leo February 08, 2023 alipokuwa Mgeni rasmi akiwamwakilisha Meya wa Manispaa hiyo katika zoezi la upandaji wa Miti eneo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma ikiwa ni mwendelezo wa kufanya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kuwa ya Kijani


Akihutubia wafanyakazi wa Hospitali hiyo Mgeni rasmi huyo amesema Manispaa ya Kigoma/Ujiji inaendelea kutekeleza Maagizo yaliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais ya Kila Halmashauri kuhakikisha inaitikia zoezi la upandaji wa Miti


Amesema kwa kipindi cha robo ya Kwanza  (Julai -Septemba 2022/2023) Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kushirikiana na Wadau na Wananchi imefanikiwa kupanda miche 34, 800 ikiwa ni miti ya Kivuli na Matunda    


Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi  Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (Maweni) Dr. Ashraf Idd Bitaliho amesema wamezindua zoezi hilo la upandaji wa miti katika eneo la Hospitali ikiwa ni kuendeleza utunzaji wa Mazingira


Kaimu Mganga mfawidhi huyo  amesema katika zoezi hilo Watumishi na wafanyakazi wa Hospitali hiyo watashiriki upandaji wa miti Mia mbili (200) na inatatunzwa na Watumishi kutoka katika idara na Vitengo vya hospitali hiyo


Manispaa ya Kigoma/Ujii imekuwa ikihamasisha Wananchi katika utunzaji wa Mazingira ikiwa ni pamoja na upandaji miti ambapo Manispaa hiyo imekuwa ikizalisha Miche ya Kisasa ya Michikichi na kuigawa bure kwa Wakulima na  Wananchi kwa lengo la   kupanda shambani, kando ya barabara na maeneo yao ya kuishi